THIS BLOG IS SPONSORED BY

THIS BLOG IS SPONSORED BY

12.02.2009

MZALENDO PUB JUMAMOSI HII


COCO BEACH MIDA YA JIONI HUWA TUNAPITA KUPUNGA UPEPO NA KULA MIHOGO





Wote hao maarufu sidhani kama nina haja ya kuwatambulisha

ITACHUKUA MUDA


KWENYE PARTY YA KUMKARIBISHA SHYROSE NYUMBANI

Aminata, Maryam Shisha, Manka, Khadija Mwanamboka, na Shyrose

12.01.2009

COUPLE OF THE WEEK

Kai na Mchumba (Steph). Tunasubiri harusi

USIKU WA DHAHABU...NAMTAFUTA NA FLOWER HUYU 'PLS CALL ME'


NENO LA SIKU

HEY DA MANKA, POLE NA MAJUKUMU.
NINA NENO NINGEPENDA KU SHARE NA WENZANGU AMBAO KWA NJIA MOJA AU NYINGINE WANAWEZA KUWA KWENYE SITUATION KAMA YANGU.
HII NI KUWASAIDIA TU WAONDOKANE NA JELA YA UJINGA KWANI KILA KITU KINAWEZEKANA ENDAPO WATAAMUA.

JITAHIDINI SANA MNAPOAMKA ASUBUHI NA KUIANZA SIKU, MSIWATAFUTE WALE WATU AMBAO MNAJUA KABISA WATAWAHARIBIA SIKU YENU, KUWACHEFUA NA KUWAFANYA MJIONE WANYONGE KAMA HAMKUSTAHILI KUZALIWA

TENA WATU KAMA HAO IKIBIDI MJITENGE NAO KABISA NA MUONDOKANE NA UTEJA WA KUWA NA MAWASILIANO NAO YA KARIBU KATIKA MAISHA YENU.

MARA NYINGINE MNAWEZA KUDHANI NI VIGUMU KWA KUTOURUHUSU MOYO KUJARIBU KUANZA MAZOEA MAPYA.
NA BILA KURUHUSU MOYO KUJARIBU KITU KINGINE KIPYA INAKUWA NI VIGUMU KUENDELEA NA MAISHA MENGINE.

HATA KAMA UMEFUKUZWA KAZI UKIKAA NA KUANZA KULIA NA KUJUTIA KAZI ILIOPITA BADALA YA KUTAFUTA KAZI MPYA INAKUWA SIO KABISA.
MARAFIKI WANAKUSALITI KILA SIKU NA BADO HUWEZI KUACHANA NAO, INAKUWA KAMA UNAOGOPA KUWAPOTEZA WAKATI UNAENDELEA KUUMIA.

MPENZI ANAKUKASHIFU NA KUKUKEJELI KILA KUKICHA NA BADO UNADHANI KUWA HUTAWEZA KUENDELEA BILA YEYE, HIYO NI KAMA JELA YA MAISHA UNAYOJITAKIA NA HAKUNA MTU YOYOTE ANAEWEZA KUKUWEKEA DHAMANA ENDAPO HUJACHAGUA KUBADILI MOYO WAKO

NI RAHISI KUSEMA KULIKO KUTENDA ILA JARIBU
NAWATAKIA SIKU NJEMA IJAYO

NI MIMI
SAFINA

QUEEN OF DANCEHALL JUMAMOSI HII ZHONG HUA GARDEN


11.30.2009

PAMOJA NA DRAMA ZA HAPA NA PALE ONYESHO LA MAPACHA WANNE LILIFANA USIKU WA JANA PALE STEREO KINONDONI

Cha kushangaza ni pale defender za polisi zilipofika kutaka kuwakamata baadhi ya wanamuziki kwa sababu zisizo julikana. Raia walikuja juu na kuwaamuru waondoke kwenda kutafuta majambazi na kuacha vijana wafanye kazi yao khaa!!!
Muziki ni burudani jamani sio seke seke

Kwenye starehe defender limefikaje?? kama ni kulinda usalama sawa. Ila kubeba wanamuziki inahusu?

Msafiri Diof alikuwepo kutoa support

Washabiki wakimtunza Diof



Defender likiondoka baada ya kushindwa kilichowaleta

Josee Mara akiwajibika jukwaani

Banza Stone nae alikuwepo kutia baraka zake

Shughuli ilivyofana

Hamza Kalala (Komandoo) alikuwepo kusindikiza wanae
MAPACHA WANNE ni band mpya inayoundwa na wanamuziki Chaz Baba, Kalala Jr, Chokoraa na Josee Mara.
Usiku wa onyesho inasemekana mpiga drums alichukuliwa na polisi dakika chache kabla hajaingia ndani, hivyo kumlazimu Kalala Jr. ambae ni muimbaji kupiga Drums kwa usiku huo.
Chaz Baba pia hakutokea na hakuna anaejua sababu
Ila alikuwepo wakati wote wa maandalizi ya show
Tunawatakia kila kheri katika safari hii ngumu

NAMTAFUTA FLOWER HUYU...POPOTE ULIPO PLS HOLLA BACK


TRAFFIC LIGHT PARTY


TAREHE YA ILE PARTY YETU....ITAKUWA 9TH DECEMBER 2009, SIKU YA JUMATANO. MUALIKO HUU NI KWA WALE AMBAO SINA NAMBA ZAO ZA SIMU AU E MAIL ADRESS ZAO

Ni matumaini yangu makubwa kuwa mtanikubalia mwaliko wangu
Nimekuwa nikiwasikia tumekuwa tukiongea, humu humu kwenye blog
Lakini wengi wenu hata kwa sura siwafahamu
Wafuatao ni baadhi ya waalikwa, list nyingine nitaitoa jumatatu ijayo....

1. MAIDA (Sijui kama uko TZ ama la, ningependa uje)

2. GK (Karibu nyumbani)

3. SAB ( nadhani huu ndio wakati muafaka uje uchukue top yako kabla haijakwapuliwa)

4. Mama Karen

5. ShAA na ShAA 2

6. JACQUE ( Tulionana Machozi lakini nahisi nimekusahau ningependa uje tukumbukane)

7. IMA (THE DESIGNER) (bwana shemeji usisahau kutuletea na mikate ya viatu)

8. DISMINDER ( Sijui ni kaka au dada ila ningependa pia kukufahamu)

9. MDAU ESIEN

10. LULU

11. KAI ROONEY

JO Sijakusahau ila najua uko shule sasa ukirudi tutafanya mambo basi
Manake ningependa sana kukuona na wewe pia.

Mpatapo mwaliko huu na kuukubali tafadhalini mniandikie email judyjaydee@yahoo.com
Au nipigie simu 255 784 700 884.
Ili niwafahamishe jinsi gani ya kupata kadi za kuingilia ndani
Asanteni na awamu ya pili ya majina itatoka wiki ijayo.

Wale wakongwe wa blog hii mnajijua na mnajua wapi tutakutana
PM punguza maswala ya safari sana tunakukosa huku jamani khaa!!¨!

Cheers
Manka Drogba

MACHOZI BAND JUMAMOSI YA TAR 5 DECEMBER 2009, TUTAKUWA YATCH CLUB MWANZA

Wakati Dec inaanza, Ratiba yetu iko kama kawaida Ijumaa Tar 4 Dec, tutakuwa Zhong Hua
Jumamosi ya Tar 5 Dec, tutaanza uwanja wa Nyamagana mchana kushuhudia (Nyamagana Cup)
Na usiku tutakuwa Yatch Club kufurahi na wapenzi wa Mwanza
Kwa Udhamini mkubwa wa Serengeti Lager na AIR Tanzania (Wings of Kilimanjaro)

MEN VS BOYS 3-0


KIBOKO YENU HUYU HAPA.... KAMA JERRY TEGETE VILE

11.28.2009

JUMAMOSI TULIKUWA KWENYE HARUSI YA EDNA NA STEVE CHACHA...MLIMANI CITY


Naona mpiga picha labda alipenda style ya nywele manake ndio nini sasa kunipiga kichwa tu

Chacha na Edna mbele ya Cake yao ya siku maalum



Wimbo wa kufungulia dance ambao waliuchagua wao ulikuwa 'NURU' we keep it local


Machozi Band

Kila kheri na baraka tele, kuna ups and downs kibao lakini kushika uzi ndio jambo la msingi sana. Kwani kuteleza si kuanguka


Mtarimbo doro huwa hauongopi lazima kuzungusha

Chacha (Bwana harusi9 ndio alinifundisha jinsi ya kufungua email adress yangu ya kwanza kabisa, sijui hata kama yeye mwenyewe anakumbuka hilo

USIKU WA DHAHABU ULIVYOKUWA ZHONG HUA GARDEN IJUMAA NA WASHINDI NIII.....

Aisha ndio aikuwa mshindi wa kwanza na ndio aliondoka na bahasha ya tshs. 100,000/= (Laki moja Cash)

Mshindi wa pili ni huyu japo hakuwepo wakati wa kutoa zawadi, kwahiyo popote utakapo pata ujumbe bidada tuwasiliane nikupatie mzigo wako.
Baada ya kuwa hakuonekana mvulana/ mwanaume aliewaka zawadi ilibidi iende hapa. Hongera pia kwa ku Graduate

Pacho Mwamba na washkaji





Nkwimba na Manka

Wadau

Joan Mbwembwe na Friends, Maryam na Graciana

Sebastian Ndege hongera pia

Prof Jay na wadogo zetu waliohitimu

Hii naona ni afadhali kuliko vile vya kupima pima hasa unapokuta counter ni foleni na wahudumu wako slow


Uzuri pia ina kamba kwahiyo unajibebea tu kama bag

11.27.2009

EID MUBARAK EVERY ONE...ONE LOVE

Nangoja mialiko ya Biriani toka kwa waislamu, Asante Sheila (Shekha Illusions)
Mwaliko wako nimeupata na kesho nitatia timu
Asante Faraji Moh'd najua wewe tutaianza wote Eid usiku wa leo

STEVE KANUMBA BADO ANALISONGESHA

Habari Jaydee

Pole na pilika na hongera kwa kazi nzuri unaoifanya.
Kwa niaba ya timu nzima ya £ovely Gamble tunapenda kuwataarifu kuwa soundtrack ya movie £ovely gamble starring Steve kanumba iko tayari na inapatikana kwenye hii link chini.Movie itakuwa tayari soon

http://www.youtube.com/watch?v=A2qD_7G8a4o

Naomba msaada wako kuiweka kwenye blog yako.
asante sana na Mungu akubariki
Frank Eyembe

PISHI JIPYA TOKA KWA CHEF MWINGINE ANAEITWA MALICK WILLIAMS

Habari ya siku dada yangu? mi mzima tupo tu tunapambana na baridi na christimas ndio inainga kwanza nawatakia wote happy eid. usione kimya bado natafuta solution nifanyeje ili niweze kufukisha utamu wa shule ya mapishi kwa walengwa? maana kiswahili bado hakijajitosheleza kwamajina ya viungo vingi tu so kama vipi basi recipe niziache tu hivyo ktk kizungu maana ni rahisi kutafsiri toka ktk kitaliano.

Leo nimekutumia picha ya huo msosi uucheki ni plate kubwa sana la chuma msosi huu ni maalumu kwa watu watatu ni nyama choma ya nguvu inayoambatana na matunda ya ladha mbalimabli na kabechi nyekundu ilyopikwa kwenye mvinyo mwekundu pia hatari sasa kwa ndugu zangu wachupa hapo nyumbani ukipata nyama choma hii na mataunda na chupa imekolea nadhani ni kurudisha chenji kwakwenda mbele lakini hapa huu ni msosi maarufu sana bar..

kazi na siku njema!!

(MALICK tutumie tu recipe maana hata kama ni za kidhungu babu wewe. Blog hii ina wajuaji kibao, tutapata tu wa kututafsiria au mnasemaje wadau??)

USIKU WA DHAHABU NI LEO SI MNAKUMBUKA??? SIO LAZIMA FULL GOLD MNAWEZA KUCHANGANYA KAMA HIVI




11.25.2009

ILE PARTY NILIOWAAMBIA AMBAYO TAREHE YAKE ITATAJWA JUMATATU IJAYO, MAMBO HAYA YOTE YATAKUWEPO.




Party itafanyika nyumbani kwetu Kimara, na maelezo zaidi yatafuata jumatatu ijayo ya tar 30 Nov....Kutakuwa na kila kitu kuanzia nyama choma mpaka pilau na supu
Tutaalika baadhi ya watu kutoka kwa followers hapo pembeni, wachangia maoni wakongwe na wapya pamoja na marafiki na wadau mbali mbali wa Machozi Band na Fans wa Captain G.
Hizo hapo mnazoona ni fruits tu, basi kachumbari zote tutaweka kama hivyo.
Hiyo ni utambulisho tu kuwapa picha mambo yatakavyokuwa
Party ni kwa watakao alikwa tu....PM. Ima The Designer vipi mtakuwepo?
Shukrani kwa Fisherman Tours

USIKU WA DHAHABU ZHONG HUA GARDEN

KWANZA KABISA VIINGILIO BEI NI ILE ILE KAMA SIKU ZOTE 5,000/=
HALAFU TUNAHAMASISHA FLOWERS NA WADAU KULIPUKA NA GOLD IPASAVYO,
KWAKUWA KUTAKUWA NA ZAWADI KUTOKA MACHOZI BAND
AMBAPO FLOWER ATAKAEPENDEZA SANA KULIKO WOTE ATAPATA FEDHA TASLIMU SHILINGI LAKI MOJA 100,000/= (KILO).

NA MVULANA / MWANAUME ATAKAEVUTIA ZAIDI ATAPATA VOUCHER YENYE THAMANI YA SH. 50,000/= (ALFU HAMSINI) YA MTANDAO WOWOTE ATAKAOKUWA ANATUMIA NA COMPLIMENTARY YA KUINGIA MACHOZI BAND KWA MUDA WA MWEZI WOTE WA DECEMBER.

ZAWADI NYINGINE NDOGO NDOGO KUTOKA ZIZZOU FASHION PIA ZITATOLEWA KWA YEYOTE YULE ATAKAE BAHATIKA.

BINTI MACHOZI PIA NITAVAA FULL GOLD KUANZIA JUU MPAKA CHINI, NA KAMA NILIVYO WAAHIDI NGUO ZANGU NITAKAZOKUWA NAVAA WIKI HIZI ZA KARIBUNI NI KUTOKA FK's FASHIONS PALE SINZA OPPOSITE VATICAN.
HUKU KICHWANI NYWELE ZIKIWA ZIMEWEKWA SAWA NA TONTOO MARCELL WA UKWELI (JENNIFER SALON 'KINONDONI')

NI MACHOZI BAND KILA IJUMAA ZHONG HUA GARDEN, KIWANJA CHA FANS WA UKWELI.
KU DANCE MWANZO MWISHO HAKUNA KUSHANGAA

FLAVA NITE JUMAMOSI YA EID EL HAJI

Tukutane hapo Mzalendo Pub

COUPLE YA WIKI


Mchelle Obama na Bwana katika Official State Dinner ya kwanza tokea Obama achukue ikulu ya USA. vazi moja swafi lilibuniwa na mbunifi asiye hata na jina kubwa ktk fani Naeem Khan Mmarekani mwenye asili ya India. Kitu cha gold hicho kimenivutia mpaka wiki hii naandaa The Golden Party Live na Machozi Band - Friday pale pale Zhong Hua Garden. ntatoa maelezo yake zaidi baadae


Mbunifu wa mitindo indian american Naeem Khan, alompendezesha Michelle Obama na vazi lake hapo juu

11.24.2009

NAOMBENI KUSAIDIWA KU DISCUSS HII MADA KUHUSU UHALISI WA MAVAZI YA KIAFRIKA


Imekuwa ikipigwa vita sana hasa kwa baadhi ya wasichana wakionekana wamevaa vi top na kuacha vitovu nje, (wala hata sio maziwa) na kuambiwa kuwa wanatembea uchi.
Na kwamba hayo sio maadili yetu....
Na hiyo inatokea pale wanapokuwa wamevaa nguo zilizobuniwa kisasa
Lakini ikitokea wameacha maungo yao wazi kwa nguo za kiasili haionekani kuwa ni neno sana, pengine huonekana kuwa ni sawa kabisa
Sio kwamba hao wanaotengeneza hizo nguo kisasa wameiga maadili yetu na kutufanya kuyachukia na kudhani maadili hayo sio yetu??
Nauliza tu jamani...
Maadili yetu ni yapi?
Kama kuna mtu ana picha zaidi za nguo za kitamaduni anisaidie hasa za Kitanzania
Mimi nadhani hawa kina Lady Gaga na kina Madona wamechukua style zetu wakazi pimp na kuzifanya kama za kwao.

Hamkawii kumkuta Kanye West kavaa mtandio wa hivi kachanganya na suruali zake za kubana hapo ndio kila mtu ataiga
Je suit ni utamaduni wetu?

KWA HABARI ZA BURUDANI NA MICHEZO TEMBELEA

http://www.shwari.com