Wednesday, May 22, 2013

LA FAMILLE 2

Habari ndugu zanguni.

Kwanza mtaniwia radhi, nimepoteza namba zote za simu mlizonitumia......Kutokana na sababu ambazo ziko nje ya uwezo wangu. Lakini majina ya wote waliochaguliwa kujiunga na La Famille 2 ninayo.

Hivyo basi naomba mniandikie tena e-mail ya namba zenu za simu tu. Ili tufahamishane ni lini tunaweza kukutana kwa mara ya kwanza pamoja...Na kupanga mikakati ya hapo baadae.

Niko katika wakati sio mzuri sana, ki muda na mambo mengine mengine...Hivyo mtanisamahe kwa kupoteza namba zenu za simu...Kichwa kimeelemewa.

Natumaini mtanielewa
Nasubiri kusikia kutoka kwenu, soon.
E-mail ni judyjaydee@yahoo.com
Natanguliza shukrani za dhati

JayDee

PROF JAY AAMUA KUVAA GWANDA - AKABIDHIWA RASMI KADI YA CHADEMA

Ilikuwa ni siku ya tar 21 May 2013 mjini Dodoma.
Ambapo msanii maarufu wa Hip Hop nchini Tanzania anaejulikana na wengi kama Prof Jay au Heavy Weight MC alipoamua kuvua gamba na kuvaa gwanda.
Uamuzi ni wake binafsi, sisi wasindikizaji tunamtakia kila kheri kwa alichokiamua









Na hizo ndio baadhi ya picha wakati wa tukio la kukabidhiwa kadi na kuwa mwanachama rasmi wa CHADEMA

Thursday, May 16, 2013

LISTENING PARTY YA ALBUM "NOTHING BUT THE TRUTH"




Mara nyingi wasanii wengi wakishamaliza kurekodi Albums
Kabla hazijafikia hatua ya kwenda sokoni.
Hufanya party inayojumuisha wadau na marafiki mbali mbali
Kupata nafasi ya kuzisikiliza nyimbo zote kabla hazijaanza kuuzwa.

Kwa maana hiyo basi
Jumamosi hii ya tarehe 18 MAY 2013
Patakuwa na Party maalum ya kusikiliza nyimbo zote zitakazopatikana kwenye album ya sita ya Lady JayDEE "Nothing But The Truth"

Hafla hiyo itafanyika NYUMBANI LOUNGE jijini Dar es salaam
Na kutakuwa na kadi za mialiko maalum 200
Ila wengine wote wanaopenda kujumuika mnakaribishwa kwa kiingilio cha sh. 5,000/= mlangoni

DJ Kim atakuwepo kukurusha Oldies kwenye Saturday Boogie Down
Kuanzia saa 3:00 usiku yaani 9:00pm mpaka watu wakitosheka

Karibuni sana mpate nafasi ya kipekee ya kusikiliza nyimbo za JayDee kwanza, kabla hazijatoka.

Wednesday, May 15, 2013

MAZUNGUMZO YA MAKUBALIANO YA LINAH NA BARNABA KAMA IFUATAVYO


Linah na Barnaba ni watoto wazuri sana
Hawana makuu ila katika hili kuna jambo limepita katikati
Ambalo liko nje ya uwezo wao na kuwalazimu wao kukanusha kuwa hatukukubaliana malipo katika show, mbali na kuwa walishachukua pia mpaka advance. Wote wawili
Wao wote wawili humuita Captain Dady:

Yafuatayo ni mazungumzo kati ya Dady na mtoto:

CAPTAIN: Mwanangu ndo hii namba yako?
LINAH:     Ndyo baba
LINAH:     Sasa baba mimi nafanya ***miln

CAPTAIN: Ok hiyo unastahili kabisa, Safari hii sina mdhamini bajeti yangu haifiki huko kwahiyo sitamudu, lakini next time nitajitahidi tuwe pamoja mwanangu.
Nitakualika VIP siku hiyo kama una nafasi, Okey!

LINAH: Ouhk but we can talk ulikuw unahwmuch?

CAPTAIN: Linah mi nna MLN*** ndugu yangu karibu tushirikiane, Am sure kuna siku nitashiriki ktk jambo lako pia. Tatizo sina mdhamini hata mmoja na napenda tuwe pamoja siku hiyo.

LINAH: Sawa dady
CAPTAIN: Thanks Kido

Siku walipotakiwa kuja ku shoot drops za TV na kuchukua advance

LINAH: Hi dady! Naweza pitia hapo nw?

Captain akampigia akamuambia aje, na wakafika wote wawili pamoja na Barnaba
Na baada ya siku hiyo, wosia ukatoka mitandaoni.
Kilichofuatia Linah alimfuata Barnaba usiku akamtupia bahasha akakimbia. "Kwa maelezo ya Barnaba".

Hivyo Barnaba akamuambia pesa kila mtu alipokea kwa mkono wake twende tu tukamrudishie dada, Dada ni muelewa atajua tu nini kimetokea. Linah akakataa akatimua zake.

Nashukuru kwa ustaarabu wa vijana hawa wawili wamekuwa waaminifu, Barnaba amezirudisha pesa zote, zake na za Linah na kuomba radhi kwa yote yaliotokea.

Gardner hajawahi kumtumia mtu yoyote anaehusika na uongozi wa THT msg kuwa eti majina ya Linah na Barnaba yaliwekwa by mistake kama ambavyo iliongelewa na moja wa viongozi wa THT

Mimi bado nawapenda sitawahukumu na ninaomba muwaelewe tu kuwa wamebanwa na hawana ujanja japo dhamira yao ilikuwa ni kushiriki show ya miaka 13.

Ila kama hakukuwa na makubaliano kama ambavyo Linah na Barnaba wameshinikizwa kuongea, walikubalije kuja mpk kuchukuliwa kwenye video camera huku wakijua wazi huo ni ushahidi tosha.....Angalia video hapo juu upate majibu

SABABU ZA MATONYA KUTOSHIRIKI SHOW YA MIAKA 13 YA LADY JAYDEE


Tetesi zinaweza kuwa za ukweli au pengine zikawa ni story za kujitungia
Lakini tetesi zinasema kuwa Matonya alipigiwa simu na wazee wa fitna mara tu waliposkia kuwa atashiriki onyesho la miaka 13 ya JayDee, wakamwambia aachane na hiyo show na kuwa watampa hela ambayo angelipwa kwenye show hiyo.
 
Na pia wangemuandalia show yake mwenyewe kubwa zaidi ya hiyo miaka 13 ya JayDee
Hizo ni fununu, ambazo hazina uhakika.
Lakini tukirudi upande wa Matonya ambae alishapokea mpaka malipo ya awali na kukubali kufanya show baadae akachomoa ni kama ifuatavyo.
 
MATONYA: Kaka kumbe tarehe ni lini kumbe:
 
CAPTAIN:    Ni Ijumaa tar 31 May 2013 kaka mwezi ujao. Tutakuwa na Linah, Jay, Barnaba, Matonya, TID, hamza Kalala
 
MATONYA: Kaka kumradh sana kuimba na band kwasasa sitoweza manake mtaitaji mandalizi makubwa ili nifanye kazi vzr_ningeomba nitizamwe ktk kazi ingine bro kumradh sana
 
CAPTAIN: Du! Nshatangaza ilikuwa kaka lakini sawa. Je ntapata ile hela kka nilipe wengine ndg yangu
 
MATONYA: Aisee hata nimekosa raha kukujuza iliswala br_kesho satano mtampa yule rafkiangu anaitwa pizon_walikuja kuleta ile pesa yagari kwaio wataileta apo apo oficen
 
CAPTAIN: Sawa kaka usijali, Nitashukuru akiileta ili huku nisipate lawama
MATONYA: ok bro
 
Mara kimyaaaaaaa....... baada ya siku mbili tatu maongezi yakaendelea
 
CAPTAIN: Naam kaka mzigo haujaletwa. Tafadhali ileteni tu hiyo hela ya watu kaka mi napewa lawama isitoshe we ni ndugu yangu usikubali hela ndogo iharibu.
 
MATONYA: Gadna aiwezi kuwa ivyo_kuna mapungufu kidgo nayaweka sawa uipate kumradh sana brother
 
CAPTAIN: Asante
 
Siku ikapita tena
 
MATONYA: Kaka kdg kunamisteki nimecheza,, lakini wiki hii haitapita mtakuona bro nimekwama kaka lakini ntajua cha haraka
 
CAPTAIN: Sijaelewa kaka ni laki **** tu kunirudishia nduguyo nilipe wasanii wengine kwani kuna tatizo au
 
MATONYA: Bro naskia haya - skutaka hata kuku2mia msg mlitaka ni2we namzigo 2 ila kunambio kdg zimekwamisha nikaona bora kukujuza kuliko kukaa kimya bro tatizo haliwezi
 
CAPTAIN: Sawa we ni ndugu yangu, basi nisaidie tu irudi hiyo advance niliyokupa ili uniepushe na lawama huku kaka. Au niende kwa bimkubwa Tanga nikalalamike? Ha haaaa haaa
 
CAPTAIN: Fanya hivyo mdogo wangu nilitaka uwepo ktk show kwa upendo tu lakini haijawa, basi nisaidie tu kurudisha hiyo advance maana nadaiwa na wasanii wengine niwape. Au sio?
 
MATONYA: Kaka nibendi ndio haya yangu kwasasa nastaki kuharibu kaziyako bora niwe mkweli.. Naswala lako halitoki kichwani bro
 
CAPTAIN: Sawa jamaa yangu, basi nisaidie ile advance irudi ili niweke mambo sawa huku, mimi sina mdhamini mpaka leo aliyetoa hela, najitegemea tu mfukoni, naomba nirudishie nilipe wengine..Au namoro matonya we ni ndugu yangu?
 
MATONYA: Sawa brother mtalisimamia soon nikuweke sawa sawa brother - akuna litakalo shindikana kaka amini 2
 
CAPTAIN: Utarudisha lini nipe uhakika kaka, niko na shida
 
Adavance ilitoka tangu mwishoni mwa mwezi April
Mazungumzo ndio kama hayo mmeyasoma
Mpaka blog inaingia mitamboni leo, advance haijarudishwa na hakuna jibu la kueleweka.
 
Wazee wa fitna kama zile tetesi ni kweli kuwa mmemzuia Matonya asifany hii show ya miaka 13 ya JayDee, na hela ameshaitumia! Kwanini msimsaidie kuirejesha mambo yaishe??
 
 
 

ALBUM YA PICHA ZA WEEK END NYUMBANI LOUNGE - MACHOZI BAND

















Tukutane tena Ijumaa kama kawaida