Sunday, April 22, 2012

CHAPATI ZA MAJI/ MAYAI

Jinsi ya kutengeneza Pancakes

Mahitaji:
Unga wa ngano 500g
Mayai 2
Sukari tablespoon 3
Chumvi teaspoon 1/2
Kitunguu  1/2         (kata vipande vidogo vidogo sana)
Hiliki 1/4 teaspoon (iliosagwa ikawa unga)
Siagi (kama Blueband au inayofanania na hiyo)

Hatua ya kwanza unapasua mayai, kisha unayakoroga katika chombo chenye nafasi ya kutosha.

ASANTENI MLIONIKUMBUSHA: 
Unaweka kitunguu mara tu baada ya mayai
 
Unaweka chumvi na sukari unaendelea kukoroga
Huku ukiweka unga wa ngano kidogo, kidogo
Na unakuwa unaongeza na maji taratibu
Huku ukiangalia uzito wa uji
Usiwe mzito sana, wala mwepesi sana
Piga piga mpaka uhakikishe mabonge bonge yote yamekwisha
Weka hiliki koroga tena

Baada ya hapo utakuwa umepata mchanganyiko wa kutengenezea Pancakes.
Weka kikaango katika moto wa wastani
Majiko yanatofautiana settings
Kwahiyo basi, kutokana na jiko lako moto uwe wa kati

Jinsi ya kuzipika:
Unaweka siagi kwenye kiaango
Unamimina unga unaacha mpk ukauke
Kabla ya kugeuza upande wa pili unapaka tena siagi
Pancake haichomwi zaidi ya dakika 3

Kwa kipimo hicho unaweza kupata Pancake 20-25
Ukitaka pungufu unakata vipimo nilivyoelezea nusu yake
Ambapo unaweza kupata Pancakes 10-12

Unasukumia na mboga yoyote unayoipenda yenye sause ya kuchovyea. Na raha yake uzile kwa mkono msafi.


6 comments:

stevie-u.s said...

Nazipenda sana hizi,sasa sitasubiri tena kupikiwa asante kwa ujuzi Jide.

Anonymous said...

Asante sana dada je unaweza ukaweka na maziwa badala ya kuweka maji?

Anonymous said...

Naona kwenye maelezo yako umesahau kuweka vitunguu au vyewewe huweki tena?

Anonymous said...

Na hicho kitunguu unaweka wapi? Dada jide.

Anonymous said...

ni sawa unaweza weka maziwa badala ya maji na kitunguu ni vizuri ukakiaanga kidogo kwenye mafuta kidogo kutoa ukakasi

Jinsi ya Kupika said...

Mhh pishi zuri na hizo chapati zaonekana nzuri sana, Tuletee pishi lingine la Chapati Za kusukuma. BIG up mama Jay Deeee.