Monday, May 21, 2012

SHUJAA FLAVIANA MATATA AGAWA MABOYA 500 YA KUJIOKOLEA MAJINI, KATIKA KUMBUKUMBU YA KUZAMA KWA MELI YA MV BUKOBA

Flaviana Matata alishindwa kujizuia na kuangua kilio wakati wa ibaada ya kumbukumbu ya miaka 16 ya ajali ya meli ya MV Bukoba alipotembelea baadhi ya makaburi ya watu waliopoteza maisha katika ajali hiyo yaliyopo Igoma jijini Mwanza, katika ajali hiyo Flaviana alimpoteza mama yake mzazi.

Flaviana Matata akikabidhi msaada wa maboya 500 kwa mwakilishi wa mkuu wa mkoa wa Mwanza, Elias Makori kulia ikiwa ni kumbukumbu ya miaka 16 ya ajali ya meli ya MV Bukoba, anayeshuhudia ni Meneja Masoko na Biashara wa Shirika la usafirishaji wa majini mkoani Mwanza la Marine Service,Kapten Obadia Nkongoki. Igoma jijini Mwanza,


Waombolezaji wengine waliofiwa na ndugu zao wakiombea marehemu wa ajali hiyo

Flaviana na wageni wakiweka  mashada kwenye makaburi ya waliofariki kwenye ajali hiyo Igoma Mwanza

9 comments:

Somebody Not Hater:.............. said...

She is so emotional jamani,me love her

Disminder orig baby said...

Mwenyezi Mungu azidi kumpa nguvu na mafanikio, huyu dada amepitia wakati mgumu sana. Hakuna kama mama lakini Mungu ajua zaid.

Keep it up dada.

annette said...

love this gal big time.....may the almighty God bless her.

stevie-u.s said...

Big up,Flaviana umeona kile ambacho wengi hawakukiona ,kwa mchango wako umeokoa roho mia tano za watanzania.

mama siyabonga said...

Hongera sana flav kwa ulichokifanya na mungu akubariki sana.

Najua how much you miss you mum but God will show you a way.

Mungu ni mwema endelea kumtegemea.

Anonymous said...

Binti huyu amefanya jambo jema sana kwa kutoa maboya kwa ajili ya wasafiri wa meli katika ziwa Victoria.Ana moyo wa upendo, Mungu ambariki na kumpa maisha mema.

Zab: 23 "Bwana ndiye mchungaji wangu sitapungukiwa na kitu."

revocatus sanka said...

Nimeipenda habari hii.Binti ameonyesha ana moyo wa upendo kwa watu, kwani asingeweza kutoa bila ya kuwa jinsi alivyo.
Mungu ambariki na amtangulie na kumuongoza katika maisha yake.

lyna wa ukweee said...

ur de best jmn Flavi.Mungu hakupe moyo uwo wakutoa.

Anonymous said...

Ndio Kifo hupangwa na Mungu Muumba,

Lakini na sisi tujitahidi kupunguza viwango vya maafa hasa hapa kwetu Tanzania:

MIFANO YA MAAFA:
1.1997-MV Bukoba
Watu zaidi ya 1,000 walifariki.
2.2002-Ajali ya Treni Dodoma
Watu zaidi ya 400 walifariki.
3.2011-SPice Island ya Zanzibar
Watu zaidi ya 3,000 walikufa.

Na ajali nyingine nyingi kila kukicha za vyombo vya usafiri kama mabasi na milipuko ya Mabomu Mbagala/Gongo la Mboto.

4.2011-Italy huko Ulaya meli ilizama walikuwepo abiria zaidi ya 1,000 lakini walikufa sio zaidi ya watu watano (5) tu!

JE, ILI KUKWEPA VIFO VYA AJALI ZA VYOMBO VYA USAFIRI TUANZE MPANGO MPYA WA KUSAFIRI KWA MIGUU NA KUTUMIA WANYAMA KAMA PUNDA?

HATA KAMA NI SAFARI YA MUSOMA AMA DODOMA?

JE KWENDA ZANZIBAR AU UKEREWE ITAKUWAJE?,,,TUTAOGELEA?

TUTAKUWA TUNALIA NA KUOMBOLEZA HADI LINI?

VIFO NA MAAFA HAVINA MAZOEA NASI TUJIFUNZE KUPUNGUZA MATOKEO NA IDADI YA VIFO KUTOKANA NA MATUKIO YA MAAFA.